KUSUKUMWA NA UPENDO. 7
Hadithi=> KUSUKUMWA NA UPENDO
Sehemu ya : 7 ***Nani ni Mungu wangu?
Mara tu nilipopata nafasi ya kuondoka nilikwenda moja kwa moja hadi chumbani kwangu. Kila kitu nilikiona kibaya. Nilichukua Biblia yangu, lakini maneno yake yalionekana yanaelea tu ukurasani. Jasho lilinitoka. Nilivua miwani yangu nikalala kitandani.
“Mambo ya kijinga”, nilisema huku nikivitazana vioo vya miwani, ambavyo nilivitumia kwa muda mrefu. Nilivichukia! Vioo vile vilinizuia kuwa hodari katika michezo. Ndugu zangu waliniita kwa majina ya utani kwa sababu ya miwani, mfano, macho manne n.k.
Niliinamisha kichwa change. Kwanini nimekasirika kwa ajili ya miwani?
Lakini mahali Fulani unisaidia. Mtume Yohana alikutana na Yesu, na baada ya hapio hakuwa mtu Yule kama zamani. Injili zote zilieleza juu ya watu waliobadilishwa na Yesu.Nami vile vile nilikuwa na hamu ya mabadiliko. Lakini moyoni nilifikiri hivi kwamba, Mungu wangu hanijali. Hakuna kitu chochote anachonifanyia.
“Nani ni Mungu wangu hasa? Yuko wapi?” nilijiuliza. “Labda ikiwa nitaendelea kusoma nitapata jibu”, nilifikiri. Lakini ilikuwa vigumu kupata msaada. Kwa kweli Biblia iliandikwa kabla hakujawa na walutheri. Ndipo nilipoona aya moja iliyonishtua – ilikuwa kama nimechomwa na nguvu ya umeme ndani yangu.
Nilikaa nikasoma tena. “Kwa kuwa mwana wa adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea,” Nilikuwa najua yote juu ya haki ya Mungu kwamba angenihukumu kufuatana na makosa yangu. Lakini hapa kulikuwa na aya ambayo ilisema kwamba, “Yesu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea. Nilijua alimaanisha nini. Lakini Yesu ataniokoaje? Na kutoka nini? angefanya muujiza?
Sasa nilianza kusoma na kuielewa aya moja kutoka waraka wa warumi;
“Kwa sababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.” Kuokoka ilikuwa kinyume cha kupotea.
“Je ni hivi tu”? nilifikiri. Kuamini tu?
Nisuingefanya mambo makubwa kwanza? Nisingelazimishwa kuishi maisha ya ukamilifu kwanza kama nilivyofundishwa kanisani.
Nilifikiri juu ya mambo yangu yote ambayo sikuyapenda kuhusu tabia yangu. Mara nyingi nilikuwa nimejaa mawazo mabaya moyoni mwangu. Yesu angeweza kubadili mambo haya?
Labda ilikuwa kweli ya kwamba alibadili maji kuwa divai miaka elfu mbili iliyopita lakini mambo haya yalinihusu mimi Bruce Olson? Nilifikiri juu ya watu wote katika injili ambao walibadilishwa na Yesu. Lakini mambo haya yalinihusu mimi? Nilijiuliza.
Nilisikia hamu kubwa moyoni kuzungumza na Yesu.
Ni kweli kwamba nilikuwa nimeomba zamani lakini yalikuwa ni maombi ya kufuatisha kanisani ambayo tulisoma kutoka kitabuni. Sasa niliona tofauti.
Nililala kitandani huku nimeinamisha usho wangu wangu chini, nikizungumza na Yesu. Yalikuwa kama mazungumzo ya kweli pamoja naye.
“Oh, Yesu”, nilisema, “nimesoma kila mtu aliyekuja kwako alivyobadilishwa. Sasa mimi nataka kubadilishwa nawe. Naomba amani na utimilifu kama Paulo na Yohana na Yakobo na mitume wengine. Naomba niokolewe na hofu yangu yote na…”
“Wakati ule niliona kule kuwamo chumbani mwangu, ni raha kabisa na kulikuwa na uwepo wa Yesu.
“Bwana nina hofu mbele yako”, niliendelea kusema. “Unajua ya kwamba sijipendi mimi mwenyewe. Kila kitu ni kama machafuko pande zote kwangu. Na ni kama machafuko ndani ya moyo wangu pia. Mungu, tafadhali unibadilishe. Siwezi kujibadili mimi mwenyewe. Na siwezi kufahamu unavyoweza kufanya kitu ndani yangu. Lakoni Yesu, ikiwa uliweza kuwabadili watu walio katika Biblia, naamini ya kwamba unaweza kunibadili hata mimi. Yesu, ninakuomba unisaidie kukufahamu. Unifanye kuwa mtu mpya”!
Wakati ule ule nilifahamu ya kwamba nimeokolewa. Kabla ya hapo nilijiona mwenye hali mbaya na dhaifu na nilikuwa nimechoka kwa ajili yangu mwenyewe. Lakini baada ya maombi yangu nilipata amani moyoni mwangu. Tena ilikuwa amani kweli kweli. Haikuwa raha tu ya kumaliza vita ndani yangu. Ilikuwa hali ya uhai, na amani na nilijiona nimefanywa hai. Nilipata hata uwezo wa kujipenda mimi mwenyewe. Kamwe sikutaka amani ile na raha ile ziondoke kwangu. Nililala kitandani nikishangaa. Nilishangaa zaidi hata sikuweza kufikiri. Niliendelea kuzungumza na Yesu kwa sababu nilijua kwamba yupo. Na kwa kuwa Yesu alikuwepo sikuwa na sababu ya kujisumbua juu ya mungu wa Kilutheri au Mungu wa wakristo wengine. Matatizo yangu yalimalizika. Yesu alikuwa Mungu wangu, Mungu wangu binafsi na nimezungumza naye sasa hivi.
____ITAENDELEA____
leo nimetoa ofa ya sehemu 2 kwa mpigo usikose sehemu ya nane kesho

No comments