GM NA HONDA WAMEZINDUA GARI LINALOJIENDESHA LENYEWE



GM na HONDA wenye uzoefu kwa zaidi yq miaka 160 wamezindua gari mpya inayojiendesha yenyewe

Gari ya umeme yenye viti sita haina usukani wala breki wala kiongeza mwendo  hakuna wipers wala side mirror. Gari hiyo haina mbele wala nyuma  kama gari za kawaida

Mwanzoni wateja hawataweza kununua gari hiyo lakini wataweza kupanda moja kwa moja kupitia program maalum

Ka kawaida gari hii imefungwa sensor maalumu kwa ajili ya ugunduzi wa  uzito na kigundua ikiwa abiria kafunga mkanda na pia kubaini ikiwa abiria ameingia au ameondoka kwenye gari

Watendaji wa gari  hiyo walisema kuliondoa gari hilo katika sifa ya gari za kawaida kunaruhusu nafasi zaidi kwa abiria kwani mlango wa kuingilia ni mpana zaidi kuliko gari za kawaida, wakati huo ina uwezo wa kuruhusu watu wawili kuingia na kutoka kwa wakati mmoja.

Gari hiyo imeundwa kwa ajili ya kutembea barabara zote za jiji na barabara kuu.

Kampuni hizo pia hazijaweka bayana ni lini zitaanza uzalishaji wa gari hiyo au ni lini itaonekana barabarani lakini walisema haitachukua muda hivi karibuni tu.

Taarifa zaidi kaa ukifatilia makala zaidi kutoka kwetu @the master pizo

No comments

Theme images by jangeltun. Powered by Blogger.